Saturday, July 12, 2014

WAZIRI WA MALI ASILI BW. NYALANDU NA WAZIRI KIVULI BW. MSIGWA MNASTAHILI PONGEZE

Habari!
   Kuna jambo limefanywa na mawaziri hawa kwa nyakati tofati,lakini wote kwa pamoja wanastahili pongezi kubwa sana,binafsi nawapongeza sana na mungu awajalie afya njema,
   Msingwa alitimiza wajibu wake kama waziri kivuli kufanya utafiti wa majangili wanaocheza na mbuga zetu kwa kigezo tu eti cha kuwa na kibali cha uwindaji ihali wanakiuka sheria na taratibu za uwindaji,bwana msingwa alionyesha ushahidi wote hadharani na watu tukaona,huu ulikuwa ni uzalendo wa hali ya juu sana ukilinganisha na kariba ya viongozi tulionao tanzania,
   Lakini pia  waziri nyarandu naye kama waziri mwenye dhamana  alifanyia kazi taarifa hiyo na hatimaye kuchukua hatua ambazo zimempendeza yoyote mpenda maendeleo tanzania,kwanza amefuta vibali vya makampuni haya uchwara na pia kuijenga upya sekta hii ya wanyama pori,ambapo sasa imekuwa mamlaka kamili ambayo inatambulika kisheria na wajumbe wa bondi watatokana na wananchi na watakuwa na mamlaka yote ya kusimamaia mamlaka hii kisheria ,,hii ni hatua nzuri na inayofaa kupongezwa.hongera sana ndugu waziri nyarandu,
     Pamoja na tofauti kubwa iliyopo baina ya viongozi hawa wa kisiasa lakini wameonyesha ukomavu wa kisiasa kwa kila mmoja kumpongeza mwenzaka kwa kazi nzuri aliyoifanya,
            VIONGOZI WENGINE TUIGE HAYA MFANO WAZIRI WA  NISHATI
BW. MSIGWA

BW. NYALANDU

TUKIWA TUNAENDELEA NA MAISHA YETU WENZETU ISRAEL NA PALESTINA WANAZIDI KUUANA.

Habari!
      Pamoja na kwamba mzozo huu ni wa siku nyingi kila binadamu aliyepo hapa duniani anaelewa vema mzozo huu,lakini kuna maswali mhimu ambayo lazima tujiulize kama raia wa dunia hii tunayeishi katika nchi tofauti na nchi hizi mbili.
     Ukiangalia kwa macho yako ya kawaida unaweza  kusema ni mzozo wa kawaida tu na usio na athali yoyote katika maisha yako na vizazi vyako kwa kuwa tu umeamua kutoifuata na kuijua historia vizuri..
         sawa pamoja na kuamua kutoifahamu historia hii,lakini bado wengi wetu tumechukua upande wa kuegemea bila kujua sababu hasa za msingi ambazo zinatufanya  tuegemee katika upande huo.iwe ni israel au palestina.lakini kuna maswali ambayo inabidi ujiulize bila kujali imani yako au rangi yako au utaifa wako......

1..Unajua asili ya uzao wako,
2.Imani yako inalitambuaje taifa la israel
3.Kwanini israel na parestina wanapigana siku zote
4.Mataifa makubwa duniani hayathubutu kuingilia mzozo huo ingali uwezo wanao
5,Unajua mipaka ya kihistoria ya mataifa haya
Jenga utaratibu wa kujisomea ili usiwe mtumwa wa fikraza wasomaji wengine duniani pia upate nafasi ya kujadili jambo kwa weledi na si kwa hisia tu..binadamu yoyote makini lazima ajue alipotoka, alipo na pale aendapo,,,,LAKINI BUSARA NI KUJUA KWANZA SAFARI YAKO KABLA HUJAANZA KUONDOKA
RAIS WA ISRAEL BWANA-BENJAMINI IKIWA NA RAIS WA MAREKANI BW. OBAMA

RAIS WA MAMLAKA YA PALESTINA BWANA- ABASI