Thursday, August 25, 2016

KUPONA KUPO TU KAMA UTAAMINI


SERIKALI,JESHI LA POLISI NA CHADEMA RAIA BADO TUNATAKA AMANI YETU,MALIZANENI MAPEMA .

Hii ni saa ya uzima na ufufuo,ni kauli ambayo hupenda kutumiwa na  Askof Gwajima ,huenda isiwe na mantiki kubwa sana kwako lakini ukiitafakari kwa kina unaweza ona umantiki wa sentensi hii.
   Leo taifa letu lipo kwenye mkanganyiko wa kauli na vitisho visivyo na mantiki katika ustawi wa taifa letu na umoja wake.ni busara kubwa iliyotumika na waasisi wa taifa hili kuweka katiba inayopaswa huheshimiwa na raia wote wa Tanzania bila kujali ukubwa,rangi,kabila,jinsia wala cheo cha raia huyo.
   Huo ni utaratibu wa karibu jamii zote za dunia,wamejiwekea katiba kama mwongozo wa maisha yao na ni dhahiri tumeona mahala ambapo katiba inaheshimiwa na watu wote amani na maendeleo mahala hapo hutawala,mifano iko hai,marekani,uingereza na nchi nyingi za ulaya,
  Lakini pia kumekuwa na utaratibu wa aina nyingine wa utawala ambao hauruhusu sana haki za raia kuwa kubwa kuzidi watawala,tunaona china,korea kusini,cuba,hii ni mifano michache tu.lakini pamoja na kutoruhusu haki hizo watawala hao wameleta maendeleo ya kweli kwa raia wao,na hiyo inawapumbaza kwa muda tu,kwa jinsi binadamu alivyoumbwa ipo siku ataidai haki hiyo ya kusikilizwa ingawaje anapewa kila asali na maziwa na mtawala wake.atataka kuongozwa siyo kutawaliwa na historia inasema hilo.
   Hapa kwetu kuna vitu ambavyo kimsingi havikufaa hata kujadiliwa na umma wa watanzania ni mambo ambao ilibidi yaamriwe na viongozi wetu tena kwa kutumia akili ya kawaida tu maana suluhu yake ipo wazi,
   Ila suluhu yake kwa point ambayo tumefika kama taifa,huenda isiwe suluhu sahihi na itatugharimu wote,watawala na watawaliwa na kuja kurudisha tena hali ya umoja wa kitaifa it will take time na huenda vizazi kadhaa hapo mbele vikakutana na matokeo mabaya ambayo viongozi wetu leo wanashindwa kutatua kwa njia ya amani na udugu.
   Polisi na serikali mna wajibika kwa asilimia kubwa,kuhakikisha amani yetu inaendelea kuwepo,lakini pia opposition kudai haki kunaendana na wajibu,timizeni wajibu na serikali itoe haki kwa raia wake kwa mjibu wa sheria na asasi zote ambazo zipo kisheria zitimize wajibu wake kwa mujibu wa taratibu na sheria zetu.
    Polisi mnao wajibu wa kulinda raia na mali zao bila kuwa na itikadi ya kuwagawa raia hawa,mkitimiza wajibu huo TANZANIA itakuwa na AMANI,ila kwa m
Askari wakiwa mazoezini
ienendo ya siku za hivi karibuni huenda kukawa na sehemu mmejikwa kidogo,rekebisheni raia bado wanawaheshimu,lakini niwape pole jeshi la polisi kwa askari wetu waliouwawa na majambazi,hili  si jambo jema na lazima raia tushiriki kuhakikisha majambazi haya yanakamatwa na sheria ichukue mkondo wake.

  UJUMBE KUTOKA KWA RAIA WA KAWAIDA TU.