Sunday, February 14, 2016

NIA YA KUIBADILISHA TANZANIA INAHITAJI NGUVU YA ZIADA YA KITAIFA

Habari,
 Jana ndugu rais aliongea na wazee wa dar es salaam,ikiwa ni ujumbe kwa taifa zima,hotuba ile inajenga utaifa na tanzania kuwa taifa la kujitegemea katika picha yake,lakini juhudi hizi la rais pamoja na baadhi ya watendaji wake hazitazaa matunda kama raia wenyewe hatutakuwa sehemu ya mabadiliko haya au mageuzi haya.
  Tutashiriki kwa kufichua waharifu walipo,lakini pia kwa kulipa kodi, zaidi kudai risiti halali ya tra katika manunuzi yetu,hili pekee litasaidia kupiga hatua za haraka katika maendeleo tunayoyataka,lakini  pia kuwe na uelewa juu ya nini hasa maana ya maendeleo,kwa viongozi wetu na raia wenyewe.huwezi kuwa na maendeleo endelevu katika taifa kama hutaweka mifumo imara katika idara zote za serikali, mifumo imara huzalisha watu makini,lakini mara nyingi watu makini huwa hawaamini katika mifumo na huona wao binafsi kama ndiyo majibu sahihi ya matatizo fulani ya raia,ni kweli kwa upande mmoja lakini wanasahau kwamba wao pia ni binadamu tu kama wengine wenye haki sawa na wengine mbele za mungu,.
    Vinginevyo namtakia kila jambo la kheri mr rais pombe achape kazi twende mbele,vija
Mr President Pombe John Magufuli
na tuwe wabunifu na tujitume katika kazi zetu "no easy way to the winning line"

Friday, February 12, 2016

SIKU 100 ZA RAIS MAGUFULI IKULU

  Habari,
     Napenda kutumia fulsa hii adimu kueleza kile kilichojitokeza katika siku 100 za mheshimiwa rais john pombe ikulu,kuna mambo mengi ameyafanya kama rais na pia baada ya kuunda serikali yake yapo yaliyofanywa na wasaidizi wake mazuri na mabaya,
   Mazuri ambayo yanaonekana kwa macho yetu ya nyama ni kwamba amepunguza safari zisizo na tija,hafla zisizo na maana japo hapo napo ipo shaka,lakini pia ameweza kuonesha ishara ya watu kuwa na nidhamu na kazi zao,ukiyachukua haya yote unaona dhamiri chanya ndani yake juu ya taifa letu,ni jambo jema na ni jambo la kujivunia.
   Mabaya yake ambayo nilazima yasemwe ili wajue na wafanyie kazi,kuminya uhuru wa bunge na kupanga kamati mhimu kimkakati,mbili kusitisha matangazo ya tbc live na kurusha edited si dalili njema kwa utawala bora,pia kutokuweka msingi wa maono yake katika katiba ya warioba bado ni tatizo lisilo na mfano,maana president pombe yeye ni binadamu anaweza kuchukuliwa na mungu muda wowote,kwa hiyo kumpata mtu kama yeye si rahisi sana japo inawezekana.kwa hiyo tunahitaji mambo yote yawekwe katika sheria mama(katiba)
   Lakini pia amezuia bunge kurushwa live lakini katika sherehe za hovyo tu za chama wanarusha live,je chama kina fedha kuliko serikali?ama chama ni mali ya uma?ama ni ubabe wa kimadaraka au kutokuwa na ufahamu juu ya utawala wa sheria?
Nyarugusu refugee camp-Tanzania
  All in all namtakia kila lililo la kheri,afanye kazi kwa bidii akumbuke katiba ndiyo msingi wa nchi kutulia na kuwa na uchumi imara,na zaidi akumbuke zanzibar ni sehemu ya jamhuri kama hakuna political stability upande mmoja wa muungano basi taifa zima litakosa utulivu,"hakuna uvunjwaji wa sheria usio na chanzo duniani,na chanzo kikuu cha uvunjwaji wa sheria ni pale serikali ikiacha kutimiza wajibu wake"