Friday, September 12, 2014

MAHUSIANO YA LEO NI KAMA NDOTO YA MCHANA

Habari wanajamvi!!!!!!
         Napenda kutumia fulsa hii kukusalimu lakini pia kuzungumza japo kwa uchache wake juu ya mahusiano yako na yangu katika dunia ya leo ya kisasa japo mimi siamini sana huu usasa.
        Leo ni siku nzuri ambayo huenda umepata mchumba mpya,mpenzi mpya,ama unayofuraha kwa sababu umekutana na mwenzako mkaamua kuwa kama mlivyozaliwa na hatimaye mkaamua muburudisha akili zenu na miili yenu,ni jambo jema kama lilifanyika kwa watu sahihi,muda sahihi na kwa usahihi wake,kama ilikuwa hivyo hongera kwa kutimiza takwa takatifu la mungu na kama ni kinyume chake poleni,
         Kwa nini tunasema  mahusiano ya leo ni kama ndoto ya mchana ni jibu ni jepesi kwa sababu mahusiano ya leo hayaaminiki hata kidogo,hata kwa wale waliojaribu kujiamini wao, wamejikuta wenzi wao hawaaminiki,kwa hiyo hii inajenga uhalali wa kwamba mahusiano ya kileo ni kama ndoto ya mchana.,lakini pia inajengwa na dhana hii, leo ukikutana na binti au kijana akatamka kwamba anakupenda,hilo neno nakupenda limebeba maana nyingine kabisa tena maana ovu,huenda anakutamani ama anataka kukuumiza tu moyo wako au anataka aondoke na roho yako,yote matatu yanawezekana na mifano yake ipo wazi kabisa na wewe unayesoma hapa ushahidi huo unao,wangapi umewadanganya,wangapi uliwambia unawapenda kumbe unawatamani,,,,,,,,,,jibu unalo na pigia mstari....
          Lakini mimi ningependa niwasihi kitu kimoja wakubwa kwa wadogo,mapenzi yapo,ngono zembe zipo na magonjwa yapo,lakini bado binadamu sisi tunaendeleza hayo yote matatu kwa kasi mpya na ari mpya.mapenzi siyo kitu kibaya mapenzi ni afya ya mtu,mapenzi yanaleta uhusiano chanya tena wenye tija ya kuongeza uzao wa dunia kama yakitumika kwa ufasaha wake.lakini mtu wa kulinda utu wako na afya yako ni jukumu lako la kwanza wewe binafsi,usiruhusu mtu mwingine aamue hatima ya afya yako wala utu wako,ulizaliwa mtu huru na unao uhuru wa kulinda afya yako na ikiwezekana ikipokwa na mtu yeyote idai kwa nguvu na mungu atakulinda.
     Leo umdhaniaye ndiye kumbe siye,basi leo katika mahusiano usitumie hisia,dhana,nenda na fact ili uwe na mwisho bora,,,wanawake waaminifu wapo na wanaume waaminifu wapo japo kwa uchache wao lakini mwombe mungu akusaidie katika hilo,,,,
             Barikiwa sana na asante kwa kusoma

No comments:

Post a Comment