Monday, March 30, 2015

ACT/WAZALENDO-MACHO YANAONA KILA LA KHERI NA SIASA ZA AFRIKA

Salama ndugu,
      Haijalishi ni kiasi gani cha maneno unasema bali ni mhimu kujua katika maneno yako yote ni maneno yapi chanya...karibu katika siasa za tanzania na afrika,
   Kama yalivyo mabara mengine basi na afrika nayo ina mambo yake ambayo hayapishani sana na mfumo wa dunia na yale yanayofanywa na dunia nyingine kwa maana ya mabara ya amerika zote,ulaya,asia na australia,lakini katika afrika siasa zake ni za aina zake yaani watu kuuana,wizi wa kura,kubambikizia kesi wagombea,mfumo dume,na zaidi hakuna haki na uwazi katika kupiga kura mpaka kutangazwa matokeo..hii ni hali halisi.na machafuko mengi chanzo ni hapo,

     ACT-chama kipya,karibuni katika uwanja ule ule wa siasa ila mkiwa na jezi mpya.matumaini ya watu ni kuona maneno yenu yanaakisi vitendo vyenu,mumewaaminisha watu hivyo na watu wanalo tumaini hilo,haijalishi ni kubwa kiasi gani au dogo kiasi gani,,maana bado mtafanya siasa za muda wenu na sababu ikiisha mtakaa pembeni mpishe kizazi kingine.

     Fanyeni lililo jema ili mkumbukwe kwa uzuri huo muda wenu "ukikwisha" friend of mine from kenya told me that.
ZITO,S TEAM
     Zito ni kiongozi mzuri na namini katika utu wake yapo mabaya as human,ila akumbuke jambo moja tu katika utendaji wake kazi,kila jambo na wakati wake na huu ni wakati wa kuitoa ccm madarakani ili ijengwe tanzania mpya,,
    Huna sababu ya kuwa wa kwanza au wa mwisho maana taifa linajengwa kila siku,shabaha ni kufanya mambo sahihi kwa masilahi ya taifa letu,,kinyume chake ni hukumu zote mbili duniani na mbinguni

WAZANZIBAR KWANINI MWAIBA NYARAKA ZENU MHIMU KWA TAIFA LENU?


Salama wanajopo,,
      Leo ni  siku tena nyingine tumshukuru mungu kwa kutuwezesha kuiona,barikiweni na bwana wapendwa..
    kuna jambo moja ambalo lazima tulisemee kama watanzania ambao tunayohaki ya msingi ya kulinda taifa letu,kwa mujibu wa gazeti la mwananchi,kuna nyaraka za serikali ya mapinduzi ya zanzibar zimeibwa na viongozi wa taifa hilo,hasa wale walioteuliwa katika ngazi hizo za kulinda na kutunza hazina hizo adimu kwa taifa lao,zimeibwa zikiwa katika chumba maalumu tena ndani ya sanduku!!!

   swali,kwanini wameiba na ni kwa masilahi ya nani?majibu ya maswali haya wezi wa nyaraka hizo wao pekee ndiyo wajuao hasa nini kiliwasukuma, japo kwa muibu wa kiongozi wa iliyokuwa kamati ya kuchunguza tuhumahizo alitoa kabisa udhibitisho kwamba,na nukuu"walirubuniwa kwa fedha na vyakula kama tende".

ikulu ya zanzibar
viongozi wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar
    Sasa kiongozi unarubuniwa kwa tende then unatoa siri za taifa lako,then after?hakuna ujuha mbaya kama kukosa uzalendo na taifa lako,,nafahamu zipo sababu nyingi amabazo zinasababisha watu kukosa uzalendo lakini hakuna sababu yoyote inayozidi amani ya taifa lako na uwepo wa taifa lako,..

Saturday, March 14, 2015

TUNAHITAJI NEEMA YA MUNGU KUPONA

Habari ndugu wanajopo,,,
        Tanzania nchi yangu,tanzania nyumbani kwangu kwa daima katika maisha yote ya huu mwili wangu,nakupenda sana,,
        Leo naona kuna jambo moja tu ambalo inabidi mungu wetu tunayemwamini aingilie kati ili nchi yetu indelee kuwa na amani na mshikamano wa kutosha na kuigwa na jamii nyingine zinazotuzunguka.
      Tanzania kwa sasa tuna mambo makubwa mawili mbele yetu ambayo yataamua amani wa taifa letu..KATIBA MPYA INAYOPENDEKEZWA NA UCHAGUZI MKUU,kupigia kura ya maoni katiba inayopendekezwa ni april 30 na uchaguzi mkuu ni october 2015,lakini mpaka sasa majimbo yaliyoandikishwa wapiga kura si zaidi ya matatu,,,hii ni hatari,tena siyo hatari ndogo kwa amani ya taifa letu,
     Ndugu rais katangaza yeye badala ya tume ya uchaguzi,ukiacha kuwageuga umoja wa vyama vya siasa yale waliyokubaliana kunduchi dar es laam na baadaye dodoma,na haki kuwageuka kwa sababu yeye ndiyo mkuu wa nchi labda aliona kuna jambo la mhimu zaidi kuliko makubalianao hayo sisi hatuwezi kujua,,,ila ninachokifahamu mimi ni lazima watanzania tumwombee rais wetu ili genge la mafisadi lisifanye mashinikizo kama haya ambayo yanaliweka taifa letu njia panda.
    Uchaguzi mkuu ni chanzo cha vurugu kubwa duniani kama kutakuwa hakuna maandalizi ya uhakika na yanayoaminika na jamii iliyokubwa,nchi nyingi za afrika zimekumbwa na machafuko kutokana na jambo hili......
 tafakari,,, chukua hatua,,,,

JESUS SAVE