Friday, April 15, 2016

NINI SABABU YA ONGEZEKO LA VIJANA MIJINI?

Salama ndugu zangu!
                Na Alex Nyaganilwa
    Hakuna siku ambayo itapita bila kumshukuru mungu,maana yeye ndiye mwenye kila aina ya uwezo mkubwa unaozungumzwa na binadamu,pekee anayestahili kuabudiwa na kutukuzwa....endelea

    Ongezeko la vijana mijini afrika si jambo geni sana,watu wanatoka vijijini na kuja mijini wakiwa na matumaini makubwa sana juu miji hiyo,lakini pindi wafikapo mijini hali huwa tofauti sana na wachache sana ndiyo hufikia ndoto zao kwa urahisi na kwa haraka,kukiwa na sababu kadhaa.
  Laakini kwanini watu wanakimbia vijijini,sababu moja kubwa ni kwamba viongozi wa bara la afrika kiwango chao cha kuwaza ni cha kawaida sana,ndio maana wakaona ni bora waweke miundo mbinu inayowagawanya raia wake kwa umbali usiokifanika,mfano unakuta mji una wakazi zaidi ya milion mbili lakini hakuna,umeme,maji,hospitali wala shule na zaidi hata barabara zenyewe hamna..hutegemei kijana wa dotcom abaki hapo kama zuzu,lazima atoke.

  Anatoka anaenda wapi?anakuja mjini ambako nako hakuna mipango miji,mtu popote anaweka kibanda analala,akiamka atakuwa machinga au atauza maandazi na pipi barabarani na maisha yake yataenda murua kabisa, maana yeye anachojua siku yake ya leo tu,kesho ni ya mungu.na saerikali zipo na zinafanya kazi,lakini kazi zao ni za kawaida si kazi za kutumia akili nyingi kama wengine duniani wafanyavyo.

  Kufikia mwaka 2050 afrika pekee itakuwa na vijana bilioni moja watakao kuwa mijini,utake usitake,wanakuja kutafuta maisha na ni haki yao kwa mujibu wa katiba,lakini pia hata nature ya uumbaji haibagui mtu kuishi popote,unaweza kuishi popote,lakini wenzetu duniani huko wamejitahidi kuweka utaratibu mzuri unaozingatia utu wa mwanadamu,ukiwa unataka kutoka sehemu moja kwenda nyingine ufuate utaratibu huo,na si kufuta mahitaji mhimu,wao wameweka mahitaji mhimu karibu mahala pote wanapoisha raia wao,maana yake nini,wao wanajua mipango miji na wanajua kasi ya ongezeko la raia wao na wanajiandaa kukabiliana nalo.

  Afrika kila jiji lina matatizo yake yanafanana.ama siku zote miundo mbinu yetu haitoshi,ujenzi holela utadhani vichaa hatupendi vitu vizuri, utadhani hatuna macho ya kuona kwamba watu wanaongezeka,ama tu serikali na viongozi walio wengi ni wezi wa mali za umma kama wao wataishi mbinguni siku zijazo,hili ni bomu amabalo litalipuka muda si mrefu na halitaacha mtu nyuma wote tutaathirika na bomu hili kwa namna moja ama nyingine.

  Ongzeko la watu linapozidi kuwa kubwa bila mipango miji,athali zake ni nyingi,magojwa ya kuambukiza,uharifu uliopitiliza,vikundi vya kigaidi,rushwa mbali mbali na zaidi vita,,,watu wakikosa mahitaji mhimu na wakiona wachache wanapata na wao hawapati lazima wadai kwa nguvu na serikali haitakubali ndio maana tunaona afrika vita za wenyewe kwa wenyewe ni nyingi sababu moja wapo ni hii ya viongozi kukosa mtazamo chanya kwa raia wake,

  Nini kifanyike,mfano kwa nchi yangu tanzania,hakuna muujiza utakuja lazima tuanze mwanzo mpya,tushirikishe watalamu na wanasiasa tupate sera bora ya makazi,ili tuanze kuweka makazi bora kila sehemu walipo wananchi ,serikali iweke mipango rafiki ya kufikisha huduma mhimu pande zote za nchi yetu ili tupunguze ongezeko la vijana mijini.nafahamu miaka mitano au kumi haitoshi kuona matokeo ya mipango bora,basi kama ni hivyo tuweke dira bora ya taifa letu,,,,,asante kwa kusoma
     

No comments:

Post a Comment