Monday, April 28, 2014

KWA NINI NDOA ZA LEO NI FULL MAJANGA???

Hakuna maendeleo yoyote kwa kujivunia ambayo unaweza kuyapata kama huna mahusiano mazuri na ndugu jamaa na marafiki ,lakini leo tuangalie kidogo tuu upande wa mahusiano ambayo yanaendeleza kizazi duniani kwa maana ya kwamba mume na mke ambao kwa hiyar yao wenyewe wanaamua kufunga ndoa na kuwa kitu kimoja, wakiwa na mawazo mengi ambayo huwenda walikuwa wanayawaza wakati wa ukapera.

   Lakini  je hizi hapa chini diyo sababu ya ndoa nyingi za vijana wa leo kuvunjika?
1-Umri wao unakuwa bado mdogo?
2-Maadili yao hayako sawa?
3-Matarajio yao  yanakuwa nje ya uwezo wao?
4-Utandawazi unarubuni bongo zao?
5-Wanatamani uhuru zaidi?
6-Wanakwepa majukumu yao kama wana ndoa?
7-Hawakuwa tayari kuingia kwenye ndoa?
8-Tamaa za kimwili ziliwalaghai?
9-Matatizo ya kiuchumi?
10-Ndoa zao zinajengwa na akili zao na si mungu?
Toeni maoni yenu wakuu ili tuone nanma ya kutoka hapa tulipo kama jamii....kwa sms 0756 787 089
WADADA WA LEO

UKUBWA DAWA!!!

Habari ndugu,najua ni kwa jinsi gani kama vijana tunapaswa kujua wajibu wetu tungali na nguvu za kutosha,lakini wajibu huo unaendana na haki za msingi za mtu,napenda kuwakumbusha kitu kimoja vijana wenzangu wa kitanzania na afrika kwa ujumla wake,
   Mtu ambaye anaweza kufanya mabadiliko katika maisha yako ni yule mtu wa ndani,nini mana ya mtu wa ndani, mtu wa ndani ni ile sauti inayokuongoza katika ukweli na usahihi wa majambo yote,na huyu si mwinginine ni roho takatifu ya mungu wako alikuumba,
  Ukisha kuweza kusikia sauti hiyo na kuitii ni dhahili kwamba utafanya mambo yote uyatmaniyo kufanya ila utafanikiwa katika yale ambayo mungu alikupa karama kwayo.miili yetu ipo ili itumike vizuri lakini ukiacha mwili ukuongoze katika maamuzi  ya maisha yako ni dhahiri hutafikia yale mafanikio ambao mungu alikusudia ufikie maana mwili,rafikiye ni yule mwovu,(shetani)wakati ukiwa na nguvu zako utumie mwili wako katika mambo yale yaliyoamuliwa kwa usahihi ili majuto isiwe sehemu ya maisha yako .....ndiyo maana tunasema ukubwa dawaaaaaaa!!!!
PAMOJA NA KUWA MSITUNI LAKINI UBUNIFU BADO UPO

Friday, April 25, 2014

TUACHE KUPEPESA MANENO KATIKA HILI!!!!

Huenda kila mmoja wetu anamawazo chanya juu ya taifa letu la tanzania,lakini ukiona kunautofauti mkubwa ambao hauna hata dalili za maridhiano,basi lazima utilie shaka hata wazo lao la kwanza la kuwa na mawazo chanya juu ya taifa letu la tanzania,
    Hakuna mahala popote dunia ambapo palikuwa na salama na palikuwa kama palivo,ila tofauti za watu katika kufikiri ndizo zilipelekea sehemu hizo kubadilika na kuwa kama palivyo,lakini mabadiliko hayo yapo ya aina mbili,mosi ni mabadiliko hanya na mbili ni mabadiliko hasi,
    Nchi zote ambazo zimekuwa na msaada mkubwa kwetu zilitofautiana katika nchi zao kwa mambo mengi lakini ilikuwa ni kwa afya ya mataifa yao,walibishana kwa hoja lakini wakitanguliza masilahi ya mataifa yao,ndio maana leo tunaona maendeleo makubwa ya kiuchumi,kijamii,kisiasa na kiroho.
    Sisi leo katika taifa letu,mchakato wa katiba una rafu ambazo zinaonyesha dhahili ubinafsi na uroho wa madaraka,na unaonyesha ni kwa jinsi gani watawala hawa hawana mapenzi mema na taifa hili,katiba siyo sera ya chama chochote cha siasa kwa sababu katiba inawalenga watanzania wote, walio na vyama na wale wasio na vyama.ccm ndicho chama tawala kina wabunge wengi na ndicho chenye dola,kwa mantiki hiyo hawa ndiyo ilibidi wawe mstari wa mbele kutetea masirahi ya wananchi kwa sababu waliaminiwa na watanzania,lakini hatuoni matarajio ya wananchi,tunaona mipasho na kupingana kwa hovyo kabisa baina ya tasisi na tasisi na baadhi ya viongozi wa serikali wanatofautiana katika baadhi ya mambo,na hii ni ishara kwamaba hawa jamaa si wamoja tena,
     Huwezi kupingana na hoja yako mwenyewe,huwezi kuwa wa kwanza kubeza kazi ya wateule wako na kama ikitokea kweli wateule wako wamepotoka pahala basi aliyepotoa ni nyule aliyewaamini na kuwateua huyo ndiye wa kunyooshewa kidole,chama cha mapinduzi kama kuna wataalamu wa sayansi ya siasa basi inabidi wajiuzuru nafasi  zao maana wameshindwa kumshauri mwenyekiti wao.lakini tukumbuke haitaishia hapo tu,tutafika mahala ambapo kutokana na mashinikizo ya viongozi wenu wakuu wa chama chenu hamtachelewa sana kujutia maamuzi ambayo mtayafanya katika andiko hili muhimu kwa taifa letu la tanzania.
    Kuna maneno mawili wanapenda sana kuyatumia ,kero za muungano,,,huhitaji hata kwenda shule kujua kwamba hizi zinazoitwa kero zinatokana na udhaifu wa watawala,hawana uthubutu wa kuamua mambo kwa tija na kwa mtazamo wa baadaye,dalili za mtu ambaye hafikiri vizuri ni kufanya maamuzi nusu nusu,taifa letu la tanzania linaongoza kwa hilo.kama nchi kama marekani katiba yao inakaribia miaka mia tatu na kitu  lakini bado ni imara,wao ni nani na sisi ni nani ni uzembe tu,
   Kama tunataka udugu wa kweli na kuenzi muungano wetu,ama kuwe na nchi moja inayoitwa tanzania na yenye rais mmoja,ama kuwe na muungano wa nchi mbili tanganyika na zanzibar alafu tuwe na shirikisho la tanzania lenye rais mmoja,,,,hakuna hoja kwamba serikali mbili zipo,kwanza serikali mbili zimetoka wapi,ulishawahi kuona wapi ndani ya nchi moja kuna amili jeshi wakuu wawili,bendera mbili,,nyimbo za taifa mbili, hiki ni kituko tu ambacho mara nyingi kinatokea katika jamii ya watu wajinga,.
       KATIBA MPYA ISIPOPATIKANA CCM WATAJIBU PAMOJA NA WINGI WAO, LAKINI HAWANA DHAMILI YA KULETA KATIBA MPYA AMBAYO ITALETA MABADILIKO MAKUBWA KATIKA ULAJI WAO,WATANZANIA TUACHANE NA UJINGA USIOKUWA NA TIJA,TUWAMBIE WAHESHIMU MAWAZO YETU KAMA WANANCHI....

Monday, April 7, 2014

SI VEMA KUDHALAU HEKIMA ZA WAASISI KIASI HIKI.

Kuna malumbano ambayo yanaendelea dodoma katika bunge la katiba tatizo likiwa ni hati ya muungano wetu wa zanzibar na tanganyika,na kitu kilichoibua malumbano hayo ni uhalali wa muungano wenyewe na uhalaili wa sahihi zilinazo halalisha hati hizo, basi ni zongo lisilo na mantiki linaloendelea pale dodoma.
  Bila kujali nini walikubaliana wazee wetu hawa,ipo hoja ya msingi ambayo inahalalisha muungano huu,tumekuwa ndugu kwa 50yrs,tumezaliana,tumeona na zaidi tumekuwa na taifa moja kwa 50yrs linaloitwa tanzania,mimi najivunia utanzania wangu,na zaidi jina tanzania linajulikana hata asili yake,
   Tatizo ni viongozi wetu ambao kila uchwao wanawaza madaraka baadala ya kuwaza kukomboa fikra za mtu mweusi,duniani pote umoja ni nguvu,na nchi zote zenye maendeleo makubwa zimeungana,kiuchumi na kijamii,marekani,urusi,ujerumani,uingereza na hata china na japani.tukiacha dhambi ya ubaguzi naamini kabisa kwa uoto wetu wa asili ambao mungu ametupa,,,tanzania itakuwa paradiso ya dunia,
   Rais wa zanzibar na rais wa jmt ni waoga na wenye uthubutu kidogo, na ndio maana waswahili wanasema uoga wako ndio umasikini wako,tupo kwenye malumbano ya muungano kutokana tu na misimamo yao kuwa hasi na isiyolenga masilahi ya taifa letu la tanzania,,,kwa miaka hamsini kilishindikana nini kuwa na serikali moja?ilikuwaje jk aruhusu zanzibar kuvunja katiba ambayo hata yeye jk na shen waliapa kuilinda?siwezi kushawishika hata kidogo,. na itawagharimu maisha yenu yote duniani na hata baada ya vifo vyenu ninyi na vizazi vyenu mkiruhusu nchi hii isambaratike eti kwa kuwa mnataka masilahi ya vyama vyenu...

      VIVA nyerere &  karume ,hekima yenu itakumbukwa na daima,mantiki ya muungano huu mliyaonesha kwa vitendo na muungwana ni vitendo.mtakumbukwa na daima

MZEE NYERERE(HAYATI)

MZEE KARUME(HAYATI)
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

Saturday, April 5, 2014

HUU NI ULIMWENGU ULIO WAZI TUJIFUNZE NA HAYA PIA.

Kwa takribani miaka kadhaa sisi kama wanadamu tumekuwa na masawli mengi ambayo hayana majibu,leo ni ulimwengu wa kisasa, utandawazi umekuwa mkubwa kiasi kwamba ukihitaji kujua jambo ni rahisi sana kujua, siamini kama wazungu hawataki tuyajue haya maana haya yapo katika tovuti mbali mbali dunia......katika makanisa mengi ya kiafrika na machapisho bali mbali tunakutana na sura ya mtu ambaye anatanabaishwa kama ni yesu kristo,lakini pamoja na kwamba yesu aliishi na wanadamu wengine ila haliko wazi sana kwa sababu ya ujuzi wa zama hizo,je picha halisi ya yesu ni ipi?na je wachungaji na watumishi wengine wa mungu wanawambia waamini wao kuwa hii picha si mwonekano halisi wa bwana yesu?  -----tuanze leo kuuliza kama wanajua watuambie ukweli,na kama hawajui kwanini hawajui,tazama hizi picha then anza udadisi wako binafsi,,,,.



JE?TUTAFIKA WANAHABARI TUNAPOPATAKA

Kuna mambo sita hivi muhimu sana ya kujiuliza kama mdau wa habari,ili ufanye kazi yako kwa ufanisi na kwa weledi wa hali ya juu,jiulize maswali haya-----1.chanzo chako cha habari. 2.kusudio la habari hiyo, 3.upatano wa habari na hali halisi 4.je umefanya utafiti 5.je habari yako inahisia yoyote,6.je habari yako ni mpya au ya zamani,,,,,,,,HAPA NDIPO IPO MISINGI YA HABARI ZOZOTE POPOTE DUNIANI,,,,je maswali haya wewe kama mteja wa habari katika vyombo mbali mbali vya habari unajiuliza kwanza kabla ya kusoma na baada ya kusoma...maana taarifa au habari ndiyo hubomoa au kujenga jamii yoyote..............jiwekee kawaida ya kuchunguza habari kabla ya kuipokea
ALEX AKIWA KAZINI KUSAKA HABARI.