Habari ndugu zangu,
Tanzanaia leo kuna jambo ambalo linaendelea na linagusa maisha ya watu wa hali ya chini kabisa na jambo hilo linalenga yale mahitaji mhimu kabisa ya binadamu, swala lenyewe linahusu makazi.
Serikali imetangaza kubomoa makazi yote ya watu nchi nzima hasa wale waliojenga sehemu zisizostahili kujengwa makazi,na tayari zoezi hili limeanza utekelezaji wake hasa katika jiji la dar es salam,ambapo katika wilaya ya kinondoni katika bonde la mkwajuni makazi zaidi ya 320 yamebomolewa,sababu zinazotolewa na serikali ukitazama kwa jicho la tatu unaona mashiko yake,lakini pia sababu hizo zinaibua maswali na hisia miongoni mwa watu juu ya utawala wa sheria na dhana ya kuheshimu utu wa mtu,
Sehemu nyingi katika taifa letu hazijapimwa,na kwa sababu tu hiyo moja inaleta maana kwamba sehemu nyingi zimevamiwa na watu,lakini je kama watu wamevamia na kuishi hapo kwa zaidi ya miaka 30,na serikali zilikuwepo na kuwa kimya,na zaidi baadhi ya watu wemepewa na hati ya makazi na serikali hizo hizo, ambapo serikali ya leo inasema hati hizo hazijulikani na ni feki.sawa tukubali hati hizo ni feki je nani anapaswa kuwajibishwa wa kwanza ni mwananchi au mtumishi wa serikali aliyetoa hati feki?utajibu wewe.
Naunga mkono kabisa kuwa, taifa linatakiwa kuwa na mipango miji inayofaa na inayoendana na ukuwaji wa dunia ,ongezeko la watu na mahitaji yake,lakini pia serikali ikumbuke kuwa serikali hizi tatu zilizopita ukiacha serikali ya mwalimu nyerere walifanya mambo ya hovyo na inabidi wawajibishwe pamoja na wananchi si haki hata kidogo mwananchi kubomolewa nyumba huku ofisa wa ardhi aliyeuza eneo husika anakuwa huru,haikubaliki.
Mwisho.....sisi wananchi pia tuache kuishi kwa mazoea,tufuate sheria na pia kila upande utimize wajibu wake kati ya serikali na raia wake.
Tuesday, December 22, 2015
RAIS MTULE WA TANZANIA NDUGU POMBE JOSEPH MAGUFULI,JE ATAENDANA NA DHANA YA (hapa kazi tu)??
Habari ndugu zangu,
Tumaini langu mu wazima wa siha njema,hatujakutana kwa kitambo kidogo katika jukwaa letu hili la kupashana habari na kushauriana mambo kadha wa kadha.
Tangu tuwe mbali mambo mengi yemetokea mengine ya kusikitisha na mengine ya furaha,niwape pole ya dhati wote waliohuzunishwa kwa lolote na pia niwatie moyo wale waliofurahi waendelee kuwa na bidii na mungu maana yeye ndiye muumba wa yote.
Siku zile tunakutana hapa tulikuwa chini ya rais jakaya mrisho kikwete kwa wale tulio tanzania na wale waliopo nje ya tanzania lakini wanajivunia utanzania wao popote walipo,ni kiongozi aliyetuongoza kwa miaka 10 na sasa ni rais mstaafu,ana yake mabaya na mazuri
na tutaendelea kumheshimu kama rais mstaafu.
Ameingia mr Pombe na kibwagizo chake cha ''hapa kazi tu'',ni jambo jema kuwa na kibwagizo cha jinsi hiyo ukilinganisha na nchi zetu hizi za kimasikini kuanzia mawazo mpaka ufanyaji kazi,ukisema hapa kazi tu kidogo inaamsha ari ya raia wake.lakini je kwa jinsi mifumo ya nchi hii ilivyo mr pombe atawezana nayo?
Swali hilo huenda likajibiwa na maelezo ambayo hayatakata kiu yako kwa haraka lakini yataongeza ari ya kutaka kujua zaidi.
----Urais wake unasitofahamu miongoni mwa watanzania ndani ya (ccm na kwa watanzania wote)
----Mr pombe ni mtendaji mzuri mno ila si kiongozi mzuri mno maana jazba ni sehemu ya madhaifu yake
-----Jambo pekee litaleta mabadiliko ya kweli katika taifa hili ni KATIBA na katika hilo mr president yupo kimya na ccm yake
-----Kwa sheria hizi mbovu na utaratibu huu mbovu wa uendeshaji wa serikali,tutajikuta tunalipa fidia kubwa sana kutokana na maamuzi ya mr president,hata ikifanya sawa ila kwa sheria hizi watatushitaki na tutalipa.
----Wahafidhina ndani ya ccm hawatakuwa tayari kuona mr pombe akigusa masilahi yao,mfano ni yale ya zanzibar na jecha salim jecha na wakubwa wenziwe.
NB-kwa jinsi hii msemo wa hapa kazi tu utapata shida katika utekelezaji wake,vinginevyo mr president namuombea kila la kheri,auvae ujasiri ili aushinde mtihani uliopo mbele yake,katiba mpya ndiyo silaha yake na tunasubiri tuone hilo na MUNGU AKUPE AFYA NJEMA UKATIMIZE MAJUKUMU YAKO VEMA;
Tumaini langu mu wazima wa siha njema,hatujakutana kwa kitambo kidogo katika jukwaa letu hili la kupashana habari na kushauriana mambo kadha wa kadha.
Tangu tuwe mbali mambo mengi yemetokea mengine ya kusikitisha na mengine ya furaha,niwape pole ya dhati wote waliohuzunishwa kwa lolote na pia niwatie moyo wale waliofurahi waendelee kuwa na bidii na mungu maana yeye ndiye muumba wa yote.
Siku zile tunakutana hapa tulikuwa chini ya rais jakaya mrisho kikwete kwa wale tulio tanzania na wale waliopo nje ya tanzania lakini wanajivunia utanzania wao popote walipo,ni kiongozi aliyetuongoza kwa miaka 10 na sasa ni rais mstaafu,ana yake mabaya na mazuri
na tutaendelea kumheshimu kama rais mstaafu.
Ameingia mr Pombe na kibwagizo chake cha ''hapa kazi tu'',ni jambo jema kuwa na kibwagizo cha jinsi hiyo ukilinganisha na nchi zetu hizi za kimasikini kuanzia mawazo mpaka ufanyaji kazi,ukisema hapa kazi tu kidogo inaamsha ari ya raia wake.lakini je kwa jinsi mifumo ya nchi hii ilivyo mr pombe atawezana nayo?
Swali hilo huenda likajibiwa na maelezo ambayo hayatakata kiu yako kwa haraka lakini yataongeza ari ya kutaka kujua zaidi.
----Urais wake unasitofahamu miongoni mwa watanzania ndani ya (ccm na kwa watanzania wote)
----Mr pombe ni mtendaji mzuri mno ila si kiongozi mzuri mno maana jazba ni sehemu ya madhaifu yake
-----Jambo pekee litaleta mabadiliko ya kweli katika taifa hili ni KATIBA na katika hilo mr president yupo kimya na ccm yake
-----Kwa sheria hizi mbovu na utaratibu huu mbovu wa uendeshaji wa serikali,tutajikuta tunalipa fidia kubwa sana kutokana na maamuzi ya mr president,hata ikifanya sawa ila kwa sheria hizi watatushitaki na tutalipa.
----Wahafidhina ndani ya ccm hawatakuwa tayari kuona mr pombe akigusa masilahi yao,mfano ni yale ya zanzibar na jecha salim jecha na wakubwa wenziwe.
NB-kwa jinsi hii msemo wa hapa kazi tu utapata shida katika utekelezaji wake,vinginevyo mr president namuombea kila la kheri,auvae ujasiri ili aushinde mtihani uliopo mbele yake,katiba mpya ndiyo silaha yake na tunasubiri tuone hilo na MUNGU AKUPE AFYA NJEMA UKATIMIZE MAJUKUMU YAKO VEMA;
TUMIA VEMA NYAKATI HIZI ZA MAPUMZIKO YA KRISMAS NA MWAKA MPYA
Habari zenu ndugu,
Huenda ukawa ni mmoja kati ya watu walio karibu sana na akili yako au ukawa mbali sana na moyo wako,yote mawili yana maana kubwa sana katika maisha yako ya kila siku,msimu tunaoenda nao ni msimu wa siku kuu za krismas na mwaka mpya ,msimu ambao unahamasa nyingi sana,zifaazo kwa jamii na zile zisizofaa kwa jamii.Lazima tuhimizane kufanya yale yanayokubalika na wengi ili tutengeneze jamii yenye busara na tahaa za utu,kuna wale watakaoamua kufanya mambo mabaya kwa makusudi ya kuumiza tu wengine,labda wanataka washiriki na wengine katika maumivu yao,au wanalipiza visasi kwa siri ama wamepoteza tumaini la maisha yao kwa hiyo wanafanya lolote ili lolote litokee bila kujali matokeo yake yatakuwa hasi au chanya,watu wa jinsi hii lazima tuwaogope sana na tuwakimbie.
Huu ni wakati ambao huwezi kupima mtu kwa uharaka kiwango chake cha maisha kwa kutumia akili yako ya kawaida,maana watu wengi wamejiandaa kwa mwaka mzima,kuwa na mavazi mazuri na ya bei ghali,wamejiandaa fedha kwa ajili ya kwenda sehemu za starehe na kula vyakula vya ghalama ,kwa hiyo si jambo jepesi kuwabaini watu hawa kwa akili zetu za kawaida.
Mshirikishe Mungu ili moyo wako na akili zako zienende na kutenda kwa uweza wake mwenyewe,mshirikishe mungu kwa maombi kwa kila jambo unalotaka kufanya na Mungu wetu ni mwingi wa rehema atakuonesha njia ikupasayo na utamaliza siku kuu yako kwa amani kubwa na familia yako bila majuto ya aina yoyote ,maana kila adui yako atageuka kuwa adui wa Mungu na Mungu wetu anajibu maombi yetu,
Bwana wetu yesu kristo anasema"lihubiri neno,uwe tayari,wakati ukufaao na wakati usiokufaa,karipia,kemea,na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho"2 timotheo 4:2
Muwe na wakati mwema na pia msiishiwe na tumaini kwa bwana wetu yesu kristo maana yeye ndiye tumaini letu
Subscribe to:
Posts (Atom)