Friday, January 1, 2016

MWAKA 2016 NI MWAKA WA UPENYO WAKO

   Kwa  kuwa tuna wakati mwema mwingine ambao Mungu mwenyezi ametujalia, basi hatunabudi kuwa waaminifu kwa huyu mungu ili tuone kusudi la kutuacha tuendelee kuishi,maana si wote wamepata fursa hii adimu.
  Naamini kabisa kuwa kila mtu awaye anawaza kufanya jambo mwaka huu,lakini haipaswi kuwa na kiu ya kufanya jambo tu,inapaswa hiyo kiu iambatane na uthubutu wake au utayari wa kufanya hilo jambo.lakini pia kumbukumbu ikae sawa kidogo hapa,Yule aliyekupa kibali cha kuuona 2016 ndiye huyo huyo ambaye anaendesha maisha yako kiroho,na wewe umeachwa uyaendeshe kimwili tu.
    Tunapoona malengo yetu hayatimii basi tujue ya kwamba jambo hilo halijapata kibali rohoni(MUNGU)ama kwa sababu ya msingi ya kiungu au ni mavuno ya dhambi zetu ambapo baba yake ni (SHETANI).hii yote inakaziwa na ukweli kwamba maisha yetu hapa duniani ni ya muda mfupi sana kwa hiyo yatupasa tutembee katika njia inayofaa ili tufanikiwe katika malengo yetu,maana ukifanikiwa katika roho yako na utafanikiwa pia katika mambo yatamaniwayo na macho yako.

    Mwaka wa upenyo wako kama ukitembea katika kusudi la Mungu maana tayari Mungu ameonesha kusudi jema juu yako mpaka ukachaguliwa kuona 2016,kazi yako pekee ya kufanya ni kuishi maisha yanayompendeza Mungu na yasiyo chukizo kwa binadamu wenzako.
    Huenda akili na moyo wako vikawa vimetekwa na matamanio ya macho yako,lakini kuanzia leo tembea katika kusudi la mungu ili utimize malengo yako, na mwovu shetani asipate nafasi ya kukuhukumu katika matarajio yako,kata roho ya uvivu,kukataliwa,visasi,hasira,mauti.hii yote ni minyororo ambayo ukifumba macho ya kiroho kidogo shetani anakufunga kwayo.

      Barikiwa na bwana na asante kwa kusoma ujumbe huu,Mungu wetu akutendee na uende kupokea baraka zake,AMIN

No comments:

Post a Comment