Wednesday, April 13, 2016

INUA UELEWA WAKO KWA KIJIFUNZA KWA WENGINE

INUA UELEWA WAKO KWA KIJIFUNZA KWA WENGINE


Salama ndugu zangu!!
   Napenda kumshukuru Mungu mwenyezi aliyetupa nafasi ya kuiona leo,pia kuwapa pole ndugu zangu wote walio katika mateso ya dunia hii,lakini jipe moyo maana mtetezi wako yuu hai na uamzi upo juu yako leo….endelea

  Inua uelewa wako kwa kujifunza kutoka kwa wengine,ni sentensi ndefu pia yenye maana kubwa sana na urefu wenye sawia na urefu wake,pia inatafsiri uhalisia wa maisha ya binadamu ya kila siku.kujifunza kumegawanyika katika makundi mawili katika mantiki yake,na wote hapa dunia tupo katika moja ya makundi haya.

-KUJIFUNZA MAMBO CHANYA-kila binadamu aliyepewa nafasi ya kuishi anacho cha kujifunza kutoka kwa binadamu mwingine kwa lugha nyepesa tunaweza sema kila binadamu ni mwalimu wa mwenzake katika upande Fulani wa ubobevu wake katika ubongo wake.wapo watu ambao huona aibu kujinza kwa sababu wanaona aibu?yaani unayakosa maarifa chanya kwa sababu tu Fulani atanicheka au Fulani akijua atatusumbua sana kwa hiyo hutaki kutoa maarifa hayo kwa wengine kwa sababu tu utasumbuliwa kufanikiwa kwa mwingine???!hizi ndizo kesi nyingi sana katika bara letu la afrika.lakini nikutie moyo “mtu yoyote anayefikiri chanya hutenda mambo chanya”vitu vyote unavyotumia gharama kubwa kuvipata na muda mwingine vinakamilisha furaha yako, vilibuniwa na watu wanaofikiri chanya na wanaopenda kujifunza bila mipaka,kwa hiyo kama akili yako unataka ifurahie kujifunza basi anza leo “kuheshimu mawazo na vipaji vya wengine”
  Hakuna uchaguzi wenye njia moja,kila uchanguzi una machaguo zaidi ya moja, hii yote ni kipimo cha kujua ni nani hasa anajua uwezo wa akili yake na vipawa vyake tangu kuumbwa kwake,ili uchochee kipawa chako lazima ujifunze mambo chanya kwa upande huu wenye mawazo chanya,
  Unaweza kujifunza kwa njia nyingi lakini njia bora zaidi ni ile ya kusikia sauti yako ya ndani inakwambia nini na matokeo ya sauti hiyo igeuze katika vitendo na watu wakuzungukao watasema wewe si wa kawaida..kuwa mpole kiasi,yape masikio nafasi kubwa kuliko mdomo wako, kisha pongeza panapofaa kupongeza na pia toa maoni yanayofaa kwa uwazi pale inapotakiwa ,,hatimaye utakuwa mtu bora na jamii yako itasema huyu mtu si wakawaida na kwa matokeo ya mawazo yako hata baada ya kuondoka mwili wako hapa duniani bado athali zako chanya zitaishi,

 KUJIFUNZA MAMBO HASI-Mambo yote hasi ndio chanzo cha mateso na mahangaiko ya wanadamu hapa duniani,kwa hiyo kama unatenda jambo hasi mahala ulipo basi ujue kwamba kama siyo leo kwa mawazo yako na matendo yako ipo siku binadamu mwingine atapata matokeo hasi kutokana na maisha yako.
  Asilimia kubwa vitu vyote vyenye chembe ya uhasi ndani yake ndivyo vinatazamwa na kuwekwa katika vyombo vya habari,magazeti,mitandandaoni na kwingineko,lakini nini sababu?sababu kubwa binadamu wengi wanafurahia majibu ya kawaida ya maswali yao bila kuuliza maswalimhimu ya nyongeza,na watengenezaji wa mambo hayo hawajatoa nafasi ya maulizo kwa bidhaa zao au huduma zao zinazodhorotesha kiwango cha kufikiri cha mwanadamu,na afrika sisi ndio wahanga wa tatizo hili.kama hawataki kuulizwa basi kabla ya kununua huduma yake au bidhaa yake jiridhishe kwanza mwenyewe kwa masilahi yako na kizazi chako.
  Ikiwa  una uwezo wa kuuliza maswali mhimu katika kila hatua ya maisha yako,iko siku utapata jibu sahihi na litakupelekea kufanya jambo chanya.”hakuna dunia majibu sahihi ya mahitaji yako mpaka utakapojua wewe unahitaji nini”kwa hiyo kuanzia leo usiwaze hasi,maneno kama siwezi,sijui,hajui,labda Fulani,nitafanya kesho,sina uhakika, ni maneno yanayopelekea binadamu uwaze hasi,epukana nayo leo ili uipe nafasi akili yako  kujifunza.
 
  Hakuna namna bora katika kujiletea maendeleo katika dunia isiyo na huruma kama hii, lazima ufungue kurasa mpya katika ubongo wako, uwaze na kujifunza mambo chanya kutoka kwa binadamu wenzako na kutoka mawazo binafsi yanayoletwa na Mungu wako kukabili mazingira yako.na hayo ndiyo mawazo bora zaidi kupata kutokea maa
na ndiyo matokeo ya bidhaa na huduma zote hizi duniani,,,WEWE UNAWEZA ANZA LEO

  

No comments:

Post a Comment