Tuesday, January 5, 2016

MAHAKAMA YAZUIA KWA MUDA BOMOA BOMOA KINONDONI

Mahakamu kuu kitengo cha ardhi,imetoa agizo kwa serikali kusitisha bomoabomoa iliyokuwa inaendelea mpaka mchana wa tarehe wa leo 5/01/2015 katika mitaa ya magomeni na kinondoni,mpake kesi ya msingi ifikie uamuzi.
     Kwa mtazamo wangu mahakama imefanya kazi yake vizuri,lakini kesi yenyewe ya msingi  na madai yake kiukweli si ya msingi kisheria,madai ya raia hawa wahanga na mbunge wao wa kinondoni kwa tiketi ya cuf, yanapunguza makali ya tukio lenyewe lakini si msingi wa kuzuia zoezi,

  Hoja yao ya kwanza wananchi wapewe muda wa kujiandaa,hoja ya pili watu wapewe maeneo mbadala ya kuishi ili wapishe zoezi kuendelea.
     Kwa hoja hizi maana yake wakazi wenyewe wanajua maeneo wanapoishi si maeneo halali na si salama kwa maisha yao pia, kwa hulka ya serikali hii ya hapa kazi tu I hope zoezi lao litaendelea maana hata rais wetu si rafiki sana na justice.
   Lakini pia hili zuio halina urafiki na maeneo mengine yaliyowekwa x na yanayoendelea kuwekwa x katika jiji la dar es salaam na kwingineko.


             LET’S KEEP ON WAITING GUY'S ONFIRE.

Sunday, January 3, 2016

UKISHANGAA YA MAKONGORO MAHANGA UTAAMINI YA KUSADIKIKA.

Ndugu!
     Imekuwa ni kawaida kwa binadamu kuwa na mitazamo tofauti na hiyo ndiyo imeleta maana halisi ya neno maisha.bado tu mawazo yetu hayatoki sana katika siasa maana siasa ni maisha yetu ya kila siku,na siasa hii tunayoisema ndo inaamua baadaye yako.
      Huko mitandaoni kuna andiko la ndugu makongoro mahanga ambalo kihalisia ameweka mawazo yake huru juu ya ukubwa wa serikali ya mr pombe,kwamba baada ya kupunguza idadi ya wizara basi matarajio ilikuwa ni kuona idadi ya makatibu wakuu inaendana na wizara husika,lakini  hilo limekuwa tofauti wizara moja imepewa makatibu wakuu mpaka watatu,sawa kuna hoja ya msingi kuwa lazima kuwe na watu maalum ili utendaji uende kwa kasi zaidi,lakini si hoja ya udogo wa baraza au serikali yake.
Prof.Magembe --waziri wa maliasili na utalii
     Kakituko kenyewe ambako kanachekesha kidogo na huenda ikawa imevunja record ya dunia  kuwa na makatibu wakuu wawili na naibu katibu mmoja,haijaeleweka utendaji kazi wa hawa watu utakuwaje,nani hasa atakuwa msemaji wa mwisho juu ya naibu katibu huyu,sawa,huenda mawazo ya rais ni makubwa kuliko yangu,lakini bado haki ya kuhoji hili na kupatiwa jibu sahihi ni mhimu,
     Nadhani kungekuwa na katibu mkuu mmoja katika kila wizara kuendana ya idadi ya wizara,alafu kuwe na idara nyigi zenye wakurugenzi wenye taaluma husika ambao watafanya kazi chini ya katibu mkuu ambaye atakuwa oversee wa idara zote.hapo dhana ya ujenzi au uundwaji wa serikali ndogo ingeleta maana kubwa zaidi.
      Ukishangaa ya makongoro utaamini ya kusadikika,kushauri ni jambo moja kufanyia kazi ushauri ni jambo lingine hasa ukijaribu kushauri kwenye jambo litakalo kosoa maamuzi yake kiafrika hili ni jambo gumu mno.
          siku njema na asante kwa kusoma ujumbe huu

Saturday, January 2, 2016

DOA NI DOA JAPO HUENDA SI DOA BAYA

   Kuwa na aina Fulani ya kufikiri ndiko huleta tofauti ya baadhi ya tafsiri ya mambo hapa duniani,na ni jambo la kheri na ndilo jambo linaletelezea tafrani katika dunia hii.
   Doa linakuwa ni doa kutokana na jamii Fulani ya wanyama au vitu Fulani kutokuwa na mfanano unaolingana kimantiki na kimwonekano,kwa mfano katika nguo yenye rangi nyeupe katika uhalisia wake au mchanganyiko wa rangi ulio rasmi,ikatokea rangi nyingine ikaingilia rangi hizo kwa bahati mbaya au kwa makusudi basi hilo huitwa doa.
    Pia kwa binadamu kama kunajambo ambalo limekubaliwaa na jamii iliyokubwa,likaonekana ni jambo jema, akatokea mmoja wapo akaenda kinyume na uhalisia huo,basi huyo mtu anakuwa anaitia doa jamii hiyo,si kwa sababu amekosea la hasha bali ni kwa sababu ameenda kinyume na matakwa ya walio wengi.

   Hoja yangu ni nini hapa,katika serikali inayoundwa na president Pombe yapo madoa ya wazi ambayo yanaifanya serikali yake ionekane huenda ikawa ya kawaida kama serikali nyingine zilizopita na  kufanya mambo ya hovyo,kama ikiwepo tofauti basi ni ile tofauti ya kawaida ya kibinadamu ambayo kiasili lazima itokee.
   Kwa nini naamini hivi,taifa imara huwa halitegemei mtu imara ili kutengeneza future ya taifa, bali huhitaji mfumo bora na imara ambao utatengeneza watu imara,Mr Pombe ni mtu imara ambaye hakutengenezwa na mfumo imara.kwa hiyo hata yale anayoyafanya kama rais wangu,mengi ni mambo yanayofaa,lakini anayafanya yeye kama mr pombe siyo mfumo .na hii ni hatari kwa ustawi wa taifa.
    Kuna majina ya mawaziri ambao hapo awali walihusishwa na skendo mbali mabali kubwa za kifisadi, na makatibu wakuu pia,lakini hao ha leo wameaminiwa na kupewa sehemu nyeti,huenda walikiri dhambi zao na wakasamehewa hilo halijulikani, na mfumo wetu hautoi mwanya huo.haya madoa huenda si madoa mabaya labda wasiwasi wangu tu.lakini yananifanya nitazame upya dhamiri ya kuivaa nguo hii kwa mara ya pili.
   Kama mambo ya taifa yataendeshwa kwa utashi wa viongozi na si kwa mujibu wa sharia mama ambayo ni katiba,basi madoa haya yatakuwa ni madoa halisi,kama matendo ya waziri mkuu Mr Majaliwa na Mr Pombe yakiwa yanatoka mioyoni mwao kweli,basi waweke misingi hiyo kikatiba,watanzania walishatoa maoni yao lakini yalikataliwa na ccm kwa maneno na vitendo,lakini ccm ni chama cha siasa kama vyama vingine hakina mamlaka ya kukanyaga maoni ya raia,japo hili lipo kikatiba mpaka leo lakini ibara hii ilivunjwa na ccm kwa makusudi kwa malengo yao hasi juu ya taifa hili.
anilunya

    Mfano Mh Rais  ameteua mawaziri nje ya wabune wa majimbo ambao wapo kikatiba hii inadhihirisha kwamba hoja ya kutenganisha ubunge na uwaziri ni hoja ambayo inaishi vichwani mwao,ila hawataki tu,wizi wa kutisha bandarini,mabehewa feki na mengineyo, yanatimiliza kusudi la kuwa na mfumo bora ambao utazalisha viongozi waadilifu aina ya Magufuri.

    Mwisho huenda madoa haya yakageuka kuwa urembo katika nguo kwa muda, ila mmiliki wa nguo hii akibadilika bado haya yatakuwa madoa yaliyokubuhu,yes!

Friday, January 1, 2016

MWAKA 2016 NI MWAKA WA UPENYO WAKO

   Kwa  kuwa tuna wakati mwema mwingine ambao Mungu mwenyezi ametujalia, basi hatunabudi kuwa waaminifu kwa huyu mungu ili tuone kusudi la kutuacha tuendelee kuishi,maana si wote wamepata fursa hii adimu.
  Naamini kabisa kuwa kila mtu awaye anawaza kufanya jambo mwaka huu,lakini haipaswi kuwa na kiu ya kufanya jambo tu,inapaswa hiyo kiu iambatane na uthubutu wake au utayari wa kufanya hilo jambo.lakini pia kumbukumbu ikae sawa kidogo hapa,Yule aliyekupa kibali cha kuuona 2016 ndiye huyo huyo ambaye anaendesha maisha yako kiroho,na wewe umeachwa uyaendeshe kimwili tu.
    Tunapoona malengo yetu hayatimii basi tujue ya kwamba jambo hilo halijapata kibali rohoni(MUNGU)ama kwa sababu ya msingi ya kiungu au ni mavuno ya dhambi zetu ambapo baba yake ni (SHETANI).hii yote inakaziwa na ukweli kwamba maisha yetu hapa duniani ni ya muda mfupi sana kwa hiyo yatupasa tutembee katika njia inayofaa ili tufanikiwe katika malengo yetu,maana ukifanikiwa katika roho yako na utafanikiwa pia katika mambo yatamaniwayo na macho yako.

    Mwaka wa upenyo wako kama ukitembea katika kusudi la Mungu maana tayari Mungu ameonesha kusudi jema juu yako mpaka ukachaguliwa kuona 2016,kazi yako pekee ya kufanya ni kuishi maisha yanayompendeza Mungu na yasiyo chukizo kwa binadamu wenzako.
    Huenda akili na moyo wako vikawa vimetekwa na matamanio ya macho yako,lakini kuanzia leo tembea katika kusudi la mungu ili utimize malengo yako, na mwovu shetani asipate nafasi ya kukuhukumu katika matarajio yako,kata roho ya uvivu,kukataliwa,visasi,hasira,mauti.hii yote ni minyororo ambayo ukifumba macho ya kiroho kidogo shetani anakufunga kwayo.

      Barikiwa na bwana na asante kwa kusoma ujumbe huu,Mungu wetu akutendee na uende kupokea baraka zake,AMIN